• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Waziri Mkuu asimamisha Watumishi saba Kilombero

Posted on: September 15th, 2019

Waziri Mkuu awasimamisha watumishi 7 Wilayani Kilombero

Na Andrew Chimesela - Ifakara

 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi watumishi saba wa Halmashauri za Kilombero na Ifakara Mji Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro kwa tuhuma za ubadhilifu wa zaidi ya Tsh. 1.3 Bil.  ambazo zinatokana na makusanyo ya mapato ya ndani.

Mhe. Kassim Majaliwa amewasimamisha kazi watumishi hao leo (Jumapili, Septemba 15), mwaka huu wakati akiongea na watumishi wa Halmashauri hizo akiwa katika siku yake ya kwanza ya ziara Mkoani Morogoro.

Mbali na kuwasimamisha kazi watumishi hao, pia Waziri Mkuu ameagiza watumishi wote wanaotuhumiwa kurejesha fedha wanazotuhumiwa kuzichukua ndani ya siku tatu kabla hajamaliza ziara yake mkoani humo.

Watumishi wanaotuhumiwa na sakata hilo ni pamoja na Reina Mrema ambaye anadaiwa kuchukua kiasi cha sh. milioni 298, Haile Njitango milioni 73, Linus Mdembo kiasi cha sh. milioni 2 kwa kushirikiana na Gregory Midas ambaye ni mtendaji Kata wa viwanja Sitini katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara.

Kuhusu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara Francis Ndulane ambaye ametuthumiwa kuingiziwa fedha Serikali sh. milioni sita katika akaunti yake, Waziri Mkuu ameagiza fedha hizo zirudishwe mara moja huku akitakiwa kukabidhi stakabadhi ya marejesho hayo kwa Waziri Mkuu kabla hajamaliza ziara yake mkoani hapa.

Waziri Mkuu amesema kwa mujibu wa taarifa ya mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG) kipindi cha mwaka 2016 hadi juni 2019, Katika mji wa Ifakara makusanyo yalikuwa ni bilioni 2.7 ambapo fedha iliyopelekwa banki ni shilingi bilioni 1.9 na kufanya kiasi cha shilingi milioni 727 kutokuwa na maelezo ya kutosha ya matumizi yake.

                                                                                            Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu ameagiza Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA kutoka Halmashauri ya Mji  Ifakara John Mvanga kurejeshwa kazini mara moja, kulindwa, kutobughudhiwa na kuendelea kufanya kazi katika kituo chake cha awali.

Bw. Mvanga anaelezwa kuwa ndiye aliyeibua uwepo wa ubadhilifu wa fedha zilizotajwa hapo juu na badae kusimamishwa kazi. “Mlimsimamisha kazi kwa sababu mlijua amegundua madudu yenu, lakini haisaidi, arejeshwe kazini naagiza apewe ulinzi wa kutosha.” Alisisitiza Waziri Mkuu.

                                                               John Mvanga Mkuu wa Kitengoo cha TEHAMA aliyekuwa amesimamishwa kazi

Kwa upande wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero, Waziri Mkuu amesema zaidi ya sh. milioni 600 hazijulikani zilipo huku kiasi cha shilingi milioni 98.5 zikidaiwa kuingizwa katika akaunti za watumishi wa Halamshauri hiyo bila maelezo yeyote.

                                                    Watumishi wa Halmashauri za Kilombero na Ifakara Mji pamoja na Wakurugenzi wa Halmashauri hizo

Waziri Mkuu amewataja watumishi walioingiziwa fedha hizo ni pamoja na Devid Onyango aliyechukua kiasi cha milioni 51, Elakada Kanongole milioni 36, Fork Karunde milioni 8 na Charlse Chali milioni 2.5.

                                                                                                      Waziri Mkuu akiongea na Watumishi 

Mhe. Kassim Majaliwa pamoja na kuongea na Watumishi wa Halmashauri hizo mbili za Kilombero na Ifakara Mji pia aliongea na wananchi wa Mchombe na Mlimba katika Halmashauri ya Kilombero na kesho anatarajia kuendelea na ziara yake katika Halmashauri za Malinyi na Ulanga.

MWISHO



Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.