• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

WASOMI WATAKIWA KUMUENZI MWL. NYERERE KWA VITENDO

Posted on: November 15th, 2018


Katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi (CCM) Tanzania Bara Mzee Philip Mangula amevitaka  vyuo vya elimu ya juu nchini kupika wataalamu watakao muenzi Mwl. Julius Kambarage Nyerere kwa  vitendo hasa katika kuelekea Tanzania ya  viwanda kwa kuwa wasomi wanao utaalam unaoweza kulisaidia Taifa kufika huko.


Mzee  Mangula aliyasema hayo wiki hii katika ukumbi wa Samola uliopo Chuo kikuu cha Mzumbe wakati wa kongamano la kumbukizi ya Baba wa Taifa Mwl. Nyerere ambalo lilikuwa na lengo la kujadili mambo mbalimbali aliyokuwa akiyafanya Mwl. Nyerere hususani kwenye sekta ya elimu.


Aidha Mzee Mangula alisema kuwa vyuo vya elimu ya juu ni vyombo vinavyo paswa kuwapatia wanafunzi uwezo wakuelewa na kuchakata fikra mbalimbali kwa malengo ya kujibu na kutatua changamoto na matatizo yanayoikabili jamii katika Nyanja mbalimbali kwa kuwa wasomi wanamchango mkubwa katika usitawi wa Taifa letu.


Akieleza  namna alivyo mfahamu Mwl. Nyerere na kabla na baada ya Uhuru Mzee Mangula alisema “mimi namfaham Mwalim kwakuwa nilifanyanae kazi mda wote alisistiza uzalendo, maadili, pamoja na uwajibikaji kwa nchi yetu kwa hiyo na waasa wasomi wetu kuwa wazalendo wa kweli na tuipende nchi yetu kama mwalimu”.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe S. Kebwe alieleza kuwa Mwl. Nyerere alipanda mbengu nzuri ya kutuweka pamoja watanzania bila kubaguana kiukabila, udini wala rangi kitu ambacho kimetufanya kuwa wamoja tangu uhuru hadi leo.


Pia Dkt. Kebwe aliwaasa watanzania wanao tumia mitandao ya kijamii  vibaya hadi wengine kufikia hatua ya kubeza juhudi alizofanya Baba wa Taifa kuacha mara moja  “Tusitumie mitandao kupandikiza chuki kwa watu tena kuna watu wanabeza juhudi za Mwalimu hivi hamuoni nchi nyingine zilivyo na matatizo ya ukabiala naomba kama kuna mtu wa namana hiyo aache mara moja” alisema Dkt. Kebwe.


Nae Mkurugenzi wa Shirika la utangazaji Tanzania TBC Dr. Ayoub Liyoba amesema juhudi alizofanya Mwl. Nyerere tangu uhuru, Muungano, Azimio la Arusha, Elimu ya kujitegemea na namna zilivyo wasaidia watanzania hadi leo tuna vyuo vikuu vingi ambavyo vinatoa elimu ya utaalam wa mambo mbalimbali hivyo amewaomba watanzania kuwa wazalendo wa taifa lao ili kumuenzi Mwl. Nyerere kwa vitendo.


Kumbukizi la Mwl. Nyerere hufanyika kila mwaka tarehe 14 ya mwezi Oktoba ikiwa ni kukumbuka na kuyaenzi mambo aliyoyafanya Baba wa Taifa enzi za uhai wake ambapo hufanyika midahalo mbalimbali, mwaka huu maada iliyoandaliwa na Chuo kikuu cha Mzumbe  ilikuwa  ‘’niupi mtazamo wa Mwl. Nyerere kuhusu elimu ya  juu’’

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Maafisa Ugani Morogoro watakiwa kuongeza jihudi, wapatiwa pikipiki.

    January 14, 2021
  • Mwenyekiti wa Kijiji mbaroni kwa kuuza Ardhi..

    January 13, 2021
  • RC Morogoro atembelea soko Kuu la Manispaa, atoa maelekezo.

    January 12, 2021
  • RC Morogoro achukizwa na matumizi mabaya ya michango.

    January 11, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.