• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Wakulima washilikishwe kilimo cha miwa

Posted on: December 7th, 2018

Waziri Mkuu ataka wananchi washirikishwe kilimo cha miwa shamba la Mkulazi II

Na. Andrew Chimesela – Morogoro

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amesema uwepo wa shamba la miwa la Mkulazi II utowe fursa kwa wananchi wa maeneo jirani   kulima zao hilo ili kuwaongezea kipato wananchi hao na hivyo kujikwamua na umaskini.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo Disemba 7  mwaka huu wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani Morogoro aliyoifanya kwa lengo la kutembelea shamba hilo la miwa ambalo liko Mbigiri katika Wilaya ya Kilosa.

Waziri Mkuu amesema Mkakati wa Serikali katika kukuza kilimo cha miwa na kuzalisha sukari kwa wingi imedhamiria pia kuhusisha wakulima wadogo wanaozunguka eneo lote la Mkulazi II. Amesema baada ya kutenga eneo lilnalotakiwa kulimwa pembeni yake lazima wahusishwe wakulima wadogo kusaidia kuzalisha miwa kwa ajili ya kiwanda hicho.

“Tulishanunua matrekta ambayo tulitarajia wananchi wale wangelimiwa na matrekta ya Serikali hawakufanya hivyo, kwa hiyo naamini nyie mtafanya hivyo”. Amesema Waziri Mkuu.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amezitaka Bodi zote mbili zinazoendesha shamba la Mkulazi II kuhakikisha shamba hilo linakuwa la mfano kwa mashamba mengine ya miwa hapa nchini kwa kuwa Serikali ina wataalamu wa kutosha na wenye weledi.

Awali akimkaribisha Waziri Mkuu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema Bodi ya Mkulazi na Bodi ya NSSF zimejizatiti kuona kuwa mradi huo unatekelezeka bila ya kipingamizi.

Hata hivyo Jenista amezitaka Bodi hizo kuwa na Uzalendo, maadili ya utendaji kazi na uaminifu ili mwisho mradi huo wa kilimo cha miwa ulete tija sio kwa taifa tu lakini pia kurejesha fedha za wanachama wake na kukuza uchumi wa nchi.

Naye Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba amemuomba Waziri Mkuu kusaidia kuongeza kasi ya ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha Sukari cha Mkulazi I kuanza uzalishaji wake mapema,  huku Mkuu wa Mkoa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akitumia fursa hiyo Kumuomba Waziri Mkuu kuanzisha  kituo cha kuuzia zao la korosho katika Mkoa wa Morogoro.

DKT. Kebwe amesema, Msimu huu Mkoa wa Morogoro umevuna korosho tani zaidi ya elfu tano, huku Halmashauri zote za Wilaya za Mkoa huo zimejipanga kulima zao la Korosho hivyo kuna umuhim wa kuwa na kituo hicho cha kununulia korosho.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Bodi ya Mkulanzi Holding Company Dkt. Hildelitha Msita ametaja baadhi ya changamoto za shamba la miwa la Mkulazi II  kuwa ni pamoja na kukosekana kwa miundombinu ya umeme, kutokuwa na uhakika wa mashine za kiwanda na ukosefu wa miundombinu ya umwagiliaji.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • RC SANARE AIAGIZA TAKUKURU.

    March 13, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.