• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Vitambulisho vya Wajasiliamali

Posted on: February 4th, 2019

Dkt. Kebwe awataka Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi kujipanga

Na.  Andrew Chimesela - Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe amewataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya za Mkoa huo kujipanga katika kutoa Elimu  na kuhamasisha wananchi hususan Wajasiliamali wadogo kuwa na vitambulisho vya kufanyia Biashara zao na kwamba hicho kitakuwa moja ya kigezo cha utendaji kazi wao.

Dkt. Kebwe ametoa kauli hiyo Februari 4 mwaka huu wakati wa kikao cha tathmini na kujiwekea mikakati ya kuongeza kasi ya uuzaji wa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo ambacho kilishirikisha Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa huo.

Akifunga kikao hicho ambacho pia kilikuwa ni cha kushirikishana na kupeana mbinu za kufanikisha zoezi hilo la utoaji wa vitambulisho kwa wajasiliamali wadogo, Dkt. Kebwe alisema utekelezaji wa zoezi hilo kwa viongozi litakuwa ni moja ya vigezo katika utendaji wao wa kazi.

 “sisi viongozi, vigezo viwili tu, vitambulisho na kusimamia mapato ya makusanyo kwenye Halmashauri  zetu, kwa hiyo Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi kigezo hiki kilichoongezeka kitatathmini uwezo wa ninyi viongozi..”alisema Dkt. Kebwe.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa ametoa muda hadi Februari 28 mwaka huu, kila Mkuu wa Wilaya awe amehamasisha wajasiliamali wadogo kununua vitambulisho hivyo kwani wajasiliamali wengi wanavihitaji isipokuwa wanahitaji kuongozwa mahali pa kuvipata.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Clifford Tandari ambaye kimsingi ndiye Mtendaji Mkuu wa Serikali  ngazi ya Mkoa amewataka Viongozi na Watumishi wote wa Serikali Mkoa humo kufanya kazi kwa Kushirikiana badala ya Kushindana.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Gairo Seriel Mchembe aliwatoa hofu Viongozi wa Kisiasa ngazi za Wilaya Wakiwemo Wahe. Madiwani kuwa, zoezi la wajasiliamali wadogo kulipa kodi Serikali Kuu halilengi kupunguza mapato ndani ya Halmashauri bali kuongeza mapato hayo. 

Kikao hicho kimekuja baada ya kuwepo kwa kasi ndogo ya uuzaji wa vitambulisho hivyo kwa walengwa ambapo hadi kufikia Januari, 27 mwaka huu Mkoa wa Morogoro ulikuwa umeuza vitambulisho 3,764 tu sawa na 15.056%.na kuwataka Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuongeza kasi ya uuzaji huo wa vitambulisho.

Katika Kikao hicho imeamriwa kuwa kila mfanyabiashara kwenye sekta isiyo rasmi asiruhusiwe kufanya biashara yake bila kuwa na kitambulisho kinachomruhusu kufanya biashara kama hajalia kodi TRA, ama Halmashauri, ama awe na kitambulisho cha Mjasiliamali mdogo.

MKoa wa Morogoro awali ulipata jumla ya vitambulisho 25,000 na awamu hii ya pili imepata jumla ya vitambulisho 40,000 ambavyo Mkuu wa Mkoa amevigawa tayri kwa Wakuu wa Wilaya na kufanya Mkoa mzima kuwa na vitambulisho 65,000.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Maafisa Ugani Morogoro watakiwa kuongeza jihudi, wapatiwa pikipiki.

    January 14, 2021
  • Mwenyekiti wa Kijiji mbaroni kwa kuuza Ardhi..

    January 13, 2021
  • RC Morogoro atembelea soko Kuu la Manispaa, atoa maelekezo.

    January 12, 2021
  • RC Morogoro achukizwa na matumizi mabaya ya michango.

    January 11, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.