• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Sanare aungana na wanandugu kumbukizi ya mwaka mmoja - wahanga wa moto

Posted on: August 10th, 2020

Morogoro wafanya kumbukizi ya wahanga wa ajali ya Moto

Na Andrew Chimesela – Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare leo Agosti 10, 2020 ameungana na ndugu Jamaa na marafiki wa wahanga wa ajali ya moto uliotokea kutokana na Lori la mafuta kupinduka na kuwaka moto Agosti 10 mwaka jana na kusababisha vifo vya watu 115 katika eneo la Msamvu Mkoani hapa.

Akihutubia wananchi waliofika eneo la makaburi ya Kola wakati wa kumbukizi tukio hilo, Loata Sanare pamoja na kutoa pole kwa ndugu, kwa kuwapoteza wapendwa wao, amewataka wananchi kujijengea utamaduni wa kutoa mapema  taarifa za majanga ya moto ili kuokoa maisha ya watu na mali zao kwa wakati.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare akiweka shada la maua kwenye mnara wa kumbukumbu wa makaburi ya wahanga wa moto Kola Mjini Morogoro

Mkuu huyo wa Mkoa pia ameiagiza Kamati ya Maafa ya Wilaya ya Morogoro  kuratibu na kusimamia majanga kama hayo yasitokee na kusababisha maafa makubwa kama ilivyotokea katika ajali hiyo ya moto badala yake hatua zichukuliwe mapema.

 “Aidha, naiagiza Kamati ya maafa ya Wilaya kuendelea  kusimamia na kuratibu mpango wa kuzuia majanga na kuchukua hatua ya kukabiliana nayo pindi yanapojitokeza” alisema Sanare

Pamoja na agizo hilo, Loata Sanare amewataka wamiliki wa magari makubwa ya mizigo kupanga ratiba za madereva wa magari hayo kuwa zaidi ya mmoja ili kupokezana mara mmoja wao anapochoka kuendesha ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.


Katika hatua nyingine amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wakishirikiana na Kamati inayojenga Makaburi ya wapendwa waliopoteza maisha katika ajali ya moto kuhakikisha ujenzi wa makaburi hayo unakamilika kwa wakati na kwa ubora kama maagizo ya Waziri Mkuu yalivyotolewa.

DC Morogoro naye akiweka shada la maua

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Wilbroad Mutafungwa amewataka wananchi kujiepusha na tabia ya kusogea eneo ambapo magari yamepata ajali kwa nia ovu hususan magari ya mizigo yaliyobeba mafuta, sumu au mizigo mingine hatari ili kujinusuru na janga lolote linaloweza kujitokeza katikaeneo hilo.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo (mwenye suti nyeusi picha ya juu na chini) na Sheilla Lukuba Mkurugenzi Halmashauri ya Manispaa ya Manispaa ya Morogoro wakiweka mashada

Kwa upande wao jeshi la zimamoto na uokoaji wamewataka wananchi kutoa mapema taarifa za kweli kwa jeshi hilo kupitia namba ya dharura na uokoaji 114 ambayo mwananchi halipishwi, lengo ni kulifanya jeshi hilo kufika eneo la ajali kwa wakati na kuokoa maisha ya watu na mali zao.

Kamanda wa jeshi la ziamoto na Uokoaji Mkoa wa Morogoro Goodluck Zelothe, akimkabidhi kizimia moto Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ishara ya kuwataka wananchi wote Moani humo kuwa na vizimia moto kwenye makazi yao ili kujiokoa na majanga ya moto pindi yanapotokea.

Akiongea kwa niaba ya ndugu wa marehemu Bw. Alli Ramadhani Muhenge aliwashukuru viongozi wote wa Serikali wakiongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jitihada za kushiriki kikamilifu wakati wa janga la moto lilipotokea, lakini pia kwa kuwahifadhi marehemu wao kwa kuwajengea makaburi na mnara wa kumbukumbu.

Waombolezaji 

Kwa Mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Sheilla Lukuba amesema katika ajali hiyo watu 115 walipoteza maisha wanaume wakiwa 109 na wanawake 6  na kuasbabisha majeruhi 21 wanaume wakiwa 16 na wanawake 5.

Baadhi ya majina ya watu waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea Agosti 10, 2019

Kufanyika kwa kumbukizi hiyo ni utekelezaji wa maagizo ya Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyeagiza kuwakumbuka wahanga hao kila inapofika tarehe 10 ya mwezi Agosti ya kila mwaka. 

Huu ndi mnara wa kumbukumbu uliojengwa kwenye makaburi ya wahanga wa moto katika makaburi ya Kola - Morogoro. Wapumzike kwa Amani Amen

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • RC SANARE AIAGIZA TAKUKURU.

    March 13, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.