• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC MOROGORO AWAJIA JUU WATENDAJI WA SERIKALI KUCHELEWESHA MATUMIZI YA FEDHA

Posted on: July 1st, 2020

RC Morogoro awajia juu Watendaji Kata, Kamati za Maendelo Kata.

Na Andrew Chimesela - Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ameuagiza Uongozi wa Kata ya Magadu na Kata ya Mbuyuni katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutumia fedha zilizoletwa na Serikali ndani ya miezi miwili badala ya kuendeleza malumbano na kusababisha fedha hiyo kukaa kwa muda mrefu.

Loata Sanare ametoa agizo hilo Juni 30, 2020 alipotembelea shule ya Sekondari ya SUA na kukutana na Wajumbe wa Kamati za Baraza la Maendeleo Kata ya Mbuyuni na Kata ya Magadu ambazo kila Kata inaamini kuwa shule hiyo iko katika eneo lake.

Mkuu wa Mkoa amelazimika kufika katika shule ya Sekondari ya SUA na kufanya kikao hicho kutokana na kamati hizo kushindwa kuzitumia fedha shilingi milioni 39 zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya kujenga madarasa mawili, kutokana na kuwepo kwa malumbano hayo huku kila Kata ikidai fedha hiyo iingiziwe kwenye akaunti ya Kata yake.

Katika Kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ametoa miezi miwili kwa fedha hiyo kufanya kazi iliyokusudiwa kwani haoni sababu ya malumbano hayo ambayo kimsingi yanachelewesha fedha ya Serikali kufanya kazi iliyokusudiwa.

 “huyo anayesema kwa nini utume magadu, kwa nini tume Mbuyuni sasa mnagombania nini shule ni hiyo hiyo moja, au ulitaka Mbuyuni iwe ya kwako uweze kufanya mambo yako, au ulitaka fedha ziingie magadu uweze kufanya unayoyataka, kwa sababu mimi sioni tatizo” amesema Loata Sanare.


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare (mwenye suti) akitembelea mazingira ya shule ya Sekondari ya SUA kabla ya kuanza kikao

zaidi Sanare amewaonya Watendaji wa Kata ya Magadu na Mbuyuni na wajumbe wengine ndani ya Kata hizo kwa uzembe uliofanyika ambao uligubikwa na maslahi binafsi huku akionya kuwa yeyote atakayegusa fedha hiyo ya Serikali atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Katika hatua nyingine, Sanare ameitaka Bodi ya shule ya Sekondari ya SUA kwa kipindi hiki ambapo bado kuna ugonjwa wa CORONA kutafuta uwezekano wa wanafunzi kukaa kwa nafasi wakisubiri madarasa mawili yanayojengwa na kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula kwani kuna muda mrefu kwa wanafunzi kuwepo shuleni.


Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Mbuyuni wakisikiliza kwa makini maagizo ya Mkuu wa Mkoa

Aidha, kupitia walimu wa Sekondari ya SUA Sanare  amewataka walimu wote Mkoani Morogoro kujituma katika kufanya kazi zao na kufuata taratibu na miongozo yote iliyotolewa na Serikali kupitia Wiazara husika huku akiwataka kuongeza juhudi katika kuinua matokeo ya mitihani katika shule wanazofundisha.

Kuhusu mipaka, Mkuu huyo wa Mkoa amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutambua mipaka ya shule hiyo ili kujua shule hiyo kwa sasa iko Kata gani na Kata itakayoonekana haina shule ya Sekondari iweke mikakati ya kuanza kujenga ili kutekeleza agizo la Serikali la Kata kuwa na shule ya Sekondari

Katika kikao hicho, walimu wa Sekondari ya SUA walitoa mapendekezo yao ya kubadili mfumo wa utoaji wa fedha Serikali kwenda kwenye taasisi, kwani mfumo wa sasa unasababisha migogoro mingi baina ya Madiwani na Wakuu wa Taasisi zinazolengwa kupewa fedha hizo.

Baadhi ya Walimu wa shule ya Sekondari ya SUA wakifurahia maamuzi ya kikao hicho hususan ujenzi wa Jengo la Utawala ambalo litawapa mazingira mazuri kwa kazi zao

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Sheilla Lukuba  amesema amesikitishwa na mgogoro huo na kuahidi kuwa kuanzia mwaka ujao wa fedha Ofisi yake itaanza kupeleka fedha lengwa moja kwa moja kwenye Taasisi husika bila kupitia akaunti za Kata ili kuepusha migogoro kama hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akiwapa zawadi ya fedha wanafunzi wawili wa shule ya Sekondari ya SUA baada ya kujibu vizuri namna ya kujikinga na ugonjwa wa CORONA

Mkuu wa shule, Sekondari ya SUA Bw. Festo Kayombo alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa pamoja na fedha hizo kulenga kujenga madarasa mawili na kutengeneza viti na meza kwa ajili ya wanafunzi, shule imeomba imeomba kubadili matumizi ya fedha hizo zikarabati madarasa mawili yaliyokuwa yanatumika na walimu kama Ofisi ili fedha zitakazobaki zijenge Jengo la Utawala ambalo ni hitaji muhim kwa sasa katika shule yao.

moja ya majengo ya Shule ya Sekondari ya SUA

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.