• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro atishia kuifunga Seminary ya St. Peter

Posted on: June 24th, 2020

RC MOROGORO ATAMANI KUONANA NA MAASKOFU.

Na Andrew Chimesela – Morogoro.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ameonesha dhamira ya kutaka kuonana na wamiliki wa shule ya Seminari ya Mtakatifu Petro ya Mkoani hapa inayomilikiwa na Kanisa Katoliki ili kueleza dhamira yake ya kutaka kuifunga shule hiyo kutokana na uwepo wa miundombinu chakavu pamoja na shule hiyo kutokuwa na Bodi inayokidhi vigenzo vya  Serikali.

Loata Sanare ametoa kauli hiyo Juni 20 mwaka huu alipofanya ziara ya kushtukiza katika Seminari hiyo, baada ya kupata taarifa kuwepo kwa mapungufu kuwa shule hiyo ina miundombinu chakavu na kuna migogoro ya kimahusiano baina ya uongozi wa Shule na wafanyakazi wa shule hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare (mwenye suti nyeusi) akiangalia ndoo ya maji kwa ajili ya wanafunzi wa shule hiyo kunawa mara watakapofungua shule ikiwa ni moja ya tahadhari ya kujiepusha na ugonjwa wa CORONA. kulia kwa Mhe. Sanare ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo.

Imeelezwa kuwa hali hiyo ya kuwepo changamoto ambazo hazina majibu kwa muda mrefu inatokana na shule hiyo kukosa Bodi ya shule ambayo inakidhi vigezo vilivyowekwa na Serikali.Kwa sababu hiyo, Mkuu huyo wa Mkoa amefika shuleni hapo ili kujiridhisha hali ya miundombinu pamoja na kusikiliza kero chache kutoka kwa wafanyakazi na baada ya hayo akatoa tamko la kutaka kuonana na mmiliki wa shule ambao ni Maaskofu wanaomiliki shule hiyo ili kuwaeleza  dhamira ya kutaka kuifunga shule hiyo endapo mapungufu yaliyopo hayatarekebishwa kwa wakati.

“shule haina Bodi nataka niwaambie hilo, na kama haina bodi hakuna mamlaka ya kuitwa shule….mimi nitafurahi kuonana na wamiliki wa shule ambao ni maaskofu na kuwaambia dhamira yangu ya kutaka kuifunga shule kama haitarekebishwa” alisema Loata Sanare.

Aidha, Sanare alimuagiza Mkuu wa shule hiyo kufuata miongozo ya Serikali katika uendeshaji wake na kwamba hata kama shule hiyo ni ya Binafsi ni lazima ifuate wa Serikali ikiwa ni pamoja na utendaji kazi wa bodi ya shule hiyo uwe wazi na upitie Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.Katika hatua nyingine Loata Sanare ameitaka Bodi ya shule iliyopo ikutane mara moja na kutembelea mazingira yote ya shule ili kuona na kupendekeza kwa wamiliki jambo la kufanya kwa lengo la kuboresha mazingira ya shule hiyo.

RC Morogoro akitembelea mazingira ya shule ya Mt. Petro iliyopo Mkoani humo. Katikati ni Gombera wa shule hiyo Fr. Aloyce Mwenyasi

Amesema shule hiyo ina heshima yake tofauti na shule nyingine, kwanza ni shule inayomilikiwa na Maaskofu, lakini pili, inaongozwa na Mapadre na Masista hivyo hangependa yawepo manung’uniko yoyote zaidi ya kuwa ni shule ya mfano.Nao wafanyakazi wa shule hiyo akiwemo Charles Mabiki na Isack Petro waliowawakilisha wenzao, wamesema shule hiyo ina changamoto nyingi, zikiwemo za kimahusiano yasiyoridhisha na uchakavu wa miundombinu ambapo pamoja na kutoa ushauri namna ya kuzitatua lakini ushauri wao umekuwa haufanyiwi kazi.

Baadhi ya Watumishi wa shule ya Mt. Petro wakitoa kero zao wakati Mkuu wa Mkoa alipotembelea shule hiyo.

Aidha, wamesema shule hiyo ina walimu vijana wengi  ambao bado wana ari ya kufanya kazi na ndio maana shule hiyo imekuwa ikitoa matokeo mazuri kwenye mitihani na hata kuingia kwenye kumi bora, lakini wanakatishwa tamaa na changamoto ambzo hazipewi kipaumbele katika kuzitatua huku zikiwa na athari kwa afya yao na wanafunzi. Kwa upande wake Gombera (Mkuu wa shule) hiyo Padre Aloyce Mwenyasi wa jimbo la Morogoro, amekiri kuwa shule hiyo kwa sasa ina miundombinu iliyochakaa kwa kuwa ukarabati wa mwisho ulifanyika miaka 25 iliyopita hivyo unahitajika ukarabati mwingine na kwamba atawasilisha ujumbe huo kwa maaskofu ili waweze kuyafanyia kazi maagizo aliyotoa Mkuu wa Mkoa. 

Shule ya Mtakatifu Petro ni shule ya kikatoliki na lengo la kutoa Elimu ya Sekondari kwa vijana Wakatoliki wanaotaka kuwa mapadre wa baadae mbapo  kwa sasa shule hiyo ina ina jumla ya wanafunzi 357.Shule hii inayojulikana zaidi kwa jina la St. Peter Seminary, ilianzishwa mwaka 1937 huko Ilonga Wilayani Kilosa, mwaka 1939 ilihamishiwa Bagamoyo na miaka 30 baadae ilihamishiwa hapa Morogoro mjini. Kwa sasa shule inamilikiwa na Maaskofu wa Kanisa Katoliki wa majimbo tisa (9) ya    Dar es Salaam, Morogoro, Tanga, Mahenge, Dodoma, Zanzibar, Kondoa, Ifakara na Same.

MWISHO



Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.