• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

RC Morogoro akemea ubaguzi Mashuleni

Posted on: April 27th, 2020

RC Morogoro akemea wanafunzi kubaguliwa

Na. Andrew Chimesela, Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare amekemea Watendaji wa Serikali Mkoani humo kwa kutowajibika ipasavyo kwa kuruhusu wanafunzi katika baadhi ya shule za Msingi kupata chakula cha mchana shuleni huku baadhi yao wakiwa wamefungiwa ndani ya madarasani kwa kisingizio cha wazazi au walezi wao kutotoa michango ya chakula na kuagiza kuwa kitendo hicho kisirudiwe tena kwa kuwa ni kitendo cha kibaguzi.

Loata Sanare ametoa maagizo hayo Aprili 27 mwaka huu wakati wa hafla fupi ya kupokea msaada wa bati kwa ajili ya ukarabati wa madarasa ya shule ya Msingi ya Mji Mkuu iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ambayo majengo yake yanahitaji ukarabati mkubwa ili wanafunzi wanaotumia majengo hayo kuwa na mazingira bora ya kusomea.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare (katikati) akipokea msaada wa bati 100 kutoka kwa mdau wa maendeleo Mchungaji Jerry Wyatt wa Kanisa la Faith Baptist. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo.

Amesema kuna baadhi ya shule za msingi ambapo walimu wao pamoja na Watendaji wa wengine wa Serikali wakiwemo Watendaji wa Kata kuacha wanafunzi kutoka baadhi ya shule kupata chakula cha mchana huku wanafunzi wengine wakiwa wamefungiwa ndani ya madarasa kitendo ambacho amekiita kuwa ni cha kinyama.

Amesema, haiwezekani watoto wengine wanakula chakula na wengine wanafungiwa ndani ya madarasa jambo linaloonesha kuwa viongozi wa eneo hilo hawafanyi kazi inavyopaswa kwani moja ya wajibu wao ni kuhakikisha wazazi wote wanachangia kama walivyokubaliana kwenye vikao vya kupanga michango hiyo baada ya kupata kibali cha Mkuu wa Wilaya na kutaka kitendo kisirudiwe tena.

 “Lakini suala la watoto wachache kula chakula wengine wanafungiwa madarasani  huo ni unyama ambao haukubaliki” alisema Sanare.

“Hili nalielekeza lisije likajirudia kabisa, ni mbaya, watoto huwezi kuwafungia darasani ni vizuri mkakusanya kadri mtakavyoweza , mkapika chakula kidogo kwa ajili ya watoto wote” alisistiza.

yanayoonekana kwa mbele ni majengo ya vyumba vya madarasa vinavyotakiwa kukarabatiwa ikiwa ni pamoja na kuezeka bati mpya

Naye Katibu Tawala wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo akimkaribisha Mkuu wa Mkoa kusema neno kwenye hafla hiyo alisema anapongeza jitihada zinazofanywa na Mkuu wa Mkoa za kuboresha Elimu ndani ya Mkoa huo na kwamba kazi yake kiutendaji inakuwa  nyepesi.

Aidha, Mhandisi Kobelo amesema ili kuhakikisha anakwenda na kasi ya Mkuu wake wa kazi, wajibu wake mkubwa ni kuhakikisha anaimarisha Kamati za shule za Msingi na Bodi za shule kwa upande wa shule za Sekondari ili wajue wajibu wao kikamilifu.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Sanare na Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo wakisaidiana na mafundi katika kupandisha kenchi kwenye moaj ya chumba cha Darasa la shule ya Msingi Mji Mkuu, walipofika hapo kwa ajili kupokea msaada wa bati 100.

Amesema inawezekana Bodi na Kamati hizo hazijaelewa kwa kina wajibu wao, hivyo anachokifanya sasa ni kuziwezesha kutambue wajibu wao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha wanafunzi katika shule wanazozisimamia wanakuwa katika mazingira mazuri ya kujifunzia  kitu ambacho anaendelea kukifanya.

Kwa upande wake Mdau aliyetoa msaada bati bati 100 zenye uwezo wa geji 28 kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo, Mchungaji Jerry Wyatt wa Kanisa la Faith Baptist lililopo Kola B katika Manispaa ya Morogoro, amesema yupo hapa nchini kwa muda mrefu kama Mchungaji ameguswa na mazingira yasiyo salama kwa wananfunzi hao na kuamua kutoa msaada huo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Sheilla Lukuba (watatu kulia) akionekana kumshukuru Mchungaji Jerry Wyatt kwa msaada alioutoa.

 

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.