• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Prof. Kabudi ahimiza Kilimo cha Mimea, miti dawa

Posted on: August 1st, 2020


Pror. Kabudi awataka Watanzania kuongeza juhudi katika uzalishaji wa mazao, kulima mimea dawa.


Watanzania wametakiwa kuongeza juhudi katika kuzalisha mazao yatokanayo na kilimo, Ufugaji na Uvuvi ili kuendana na hatua ya nchi yetu kuingia hatua ya uchumi wa kati.


Rai hiyo imetolewa na Prof. Paramagamba Kabudi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianao wa Afrika ya Mashariki wakati akizindua sherehe za Maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Uvuvi Kanda ya Mashariki zilizofanyika katika viwanja vya Mwl. Julius Kambaragae Nyerere katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Mkoani humo.


Prof. Kabudi amsema hivi karibuni Tanzania imeingia kwenye  Uchumi wa Kati hatua hiyo imechangiwa na Ujenzi wa Viwanda iliyofanywa na Serikali ya awamu ya Tano ikiongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.


Amesema kwa sasa viwanda vitahitaji mali ghafi hivyo ni jukumu la Wakulima, Wafugaji na Wavuvi kuongeza juhudi katika kuzalisha mazao hayo kwa kutumia teknolojia mpya ambayo wataipata kupitia Maonesho ya Wakulima na Wafugaji maarufu kama Nanenane.


Ameongeza kuwa nia ya Serikali ni kuongeza uchumi wa Taifa na wa mtu mmoja mmoja ili kupata mazao mengi na bora hivyo vema wakulima wakawa na tabia ya kutembelea maonesho hayo ili kupata Elimu mpya katika kuzalisha mazao yao.


Katika Hatua nyingine Prof. Kabudi amewataka watanzania kuanza kujielekeza katika kilimo cha mimea dawa badala ya kuendelea kulima mazao ya kawaida pekee kwa kuwa mimea dawa ina soko katika nchi nyingi hapa Duniani.


“Wakati umefika sasa kwa watanzania kuanza kulima mimea dawa au miti dawa, nawahakikishia baada ya miaka mitano ijayo Tanzania itakuwa na biashara kubwa sio Tanzania tu bali pia Duniani” alisema Prof. Kabudi.


Akijibu maombi yaliyotolewa mbele yake juu ya sherehe hizo kufanyika Kitaifa katika kanda ya Mashariki, Prof. Kabudi amesema amelichukua ombi hilo na ataliwasilisha ngazi ya Taifa na ataendelea kufuatilia ombi hilo ili mwakani Maonesho hayo ya nanenane ikiwezekana yafanyike Kanda ya Mashariki inayoundwa na Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Tanga na mwenyeji Mkoa wa Morogoro.


Maonesho ya Nanenane mwaka huu ni ya 27 tangu kuanzishwa kwake na ni ya Nne tangu yaanze kuratibiwa na Sekretarieti za Mikoa. Kaulimbiu ya maonesho ya mwaka huu ni “Kwa maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi chagua Viongozi Bora 2020” yakibeba tukio la kitaifa la kuwepo kwa Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

 

MWISHO.




Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.