• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

Posted on: February 26th, 2021

Mkoa wa Morogoro kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa Utalii,  mamlaka za uhifadhi na kituo cha utangazaji ITV wamewasilisha mpango mkakati wa kuufanya Mkoa huo kuwa wa kiutalii kwa kuainisha vivutio vyote vya utalii vilivyopo katika Halmashauri tisa za Mkoa huo.

Mawasilisho hayo yamefanyika leo Februari 26 mwaka huu katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kikao hicho ni mahususi kwa ajili ya kukuza na kuendeleza utalii na vivutio vingine Mkoani humo.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kikao hicho amesema lengo kubwa la kikao hicho ni kuweka uelewa wa pamoja wa vivutio vilivyopo katika Mkoa huo, kutambua changamoto na kuweka mikakati ya kuendeleza utalii katika Mkoa  na taifa kwa ujumla.

Loata Sanare amesema moja ya lengo la jitihada zinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli za kuendeleza utalii lengo ni kuongeza pato la nchi na kukuza ajira katika Nyanja zote hususan katika usafirishaji, Kilimo, biashara na viwanda na miundombinu mingine.

Aidha, Loata Sanare amebainisha kuwa hadi sasa sekta ya utalii inachangia zaidi ya asilimia 17 ya pato la taifa na kiasi kidogo ukilinganisha na utajiri wa vivutio na rasilimali vingine vilivyopo katika Mkoa wa Morogoro.

Akitoa taarifa ya hali ya vivutio vya utalii katika Mkoa huo, Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Emmanuel Kalobelo amesema licha ya fursa nyingi zilizopo katika Mkoa huo, utalii ulikuwa haujapewa kipaumbele hivyo kwa sasa wametambua vivutio vyote vya utalii na kuandaa mwongozo ambao utahusisha mbuga za wanyama na utamaduni yaani vivutio vya asili.

‘’Moja ya fursa ambayo tulikuwa hatujaitumia katika Mkoa wetu ni utalii ambayo kama Mkoa tumejipambanua kwamba tuna maeneo mengi ya utalii, tumeunda kamati kuweza kuandaa andiko la mwanzo la kuangalia ni kwa namna gani tunaweza kuwa na mwongozo wa utalii katika Mkoa wetu wa Morogoro’’ amesema Kalobelo.

Mhandisi Kalobelo amesema kuwepo kwa kikao hicho ni pamoja na kutekeleza maelekezo ya ilani ya uchaguzi ya Chama kilichopo madarakanai - CCM ya mwaka 2020 ambayo imeelekeza katika kipindi hiki kuhimiza masuala ya utalii ili kuongeza pato la taifa.

Sambamba na hayo, Mhandisi Kalobelo ametoa wito kwa wadau wa kikao hicho kufikiria  namna  Mkoa wa Morogoro unavyoweza kujikuza kitalii kutokana na vyanzo vingi vya kitalii vilivyopo katika Mkoa huo hali itakayopelekea kuinua uchumi wa wananchi wake, Mkoa na Taifa kwa kwa ujumla.

Wakiwasilisha taarifa za vivutio vinavyopatikana katika Mkoa wa morogoro wadau waliohudhuria katika kikao hicho akiwemo Afisa Mhifadhi daraja la pili Mikumi kutoka hifadhi ya taifa ya Mikumi Samwel Mguhachi, amesema hifadhi hiyo ina wanyama watano wakubwa wanaopendwa kuangaliwa akiwemo Simba, nyati, Tembo, Chui na Kiboko.

Akibainisha changamoto zilizopo katika sekta ya utalii Mkoani Morogoro kwa lengo la kutatuliwa ili kuwatengenezea mazingira rafiki watalii kutoka ndani na nje ya Mkoa huo Afisa Wanyamapori wa Mkoa wa Morogoro Joseph Chuwa amesema kuna uwekezaji mdogo katika utalii hususan katika makampuni ya kusafirisha watalii.

Pia, Chuwa amebainisha changamoto nyingine kuwa ni ubovu wa miundombinu, kutotangazwa vivutio vya utalii, uharibifu wa mazingira unaotishia uhai wa vivutio vilivyokuwepo na upungufu wa fedha kwa ajili ya kuendesha shughuli za kiutalii.


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • RC SANARE AIAGIZA TAKUKURU.

    March 13, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.