• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

MABARAZA YA WAFANYAKAZI NI KIUNGO MUHIM

Posted on: July 20th, 2020

SERIKALI YASEMA MABARAZA YA WAFANYAKAZI NI KIUNGO MUHIM

 

Na Andrew Chimesela – Morogoro

 

Serikali imesema itaendelea kujali na kuzingaztia utaratibu uliopo wa kuwa na Mabaraza ya Wafanyakazi kwa kila Taasisi kwa kuwa mabaraza hayo ni kiunganishi muhim kati ya Menejimenti na Wafanyakazi ndani ya Taasisi za Serikali.

Hayo yamesemwa Julai 20 mwaka huu na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare kwa niaba ya Dkt. Philip Mpango, Waziri wa  Fedha na Mipango, alipokuwa akifungua kikao cha kwanza cha Baraza Kuu la Nne la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kilichofanyika katika Ukumbi wa TAFORI Mkoani hapa.

Amesema lengo la Serikali katika Taasisi zake ni kutaka kuleta mafanikio katika Nyanja zote zinazofanywa na wafanyakazi wake hivyo ili kufikia mafanikio chanya ni lazima kuwa na mahusiano mazuri baina ya waajiri na waajiriwa pamoja na kuwashirikisha Wafanyakazi mambo muhimu yanayofanywa na Taasisi husika.

“mathumuni ya kuwashirikisha watumishi ni kutaka kujadili na kuishauri serikali kuhusu masuala yanayohusu maslahi ya ajira mahali pa kazi kwa lengo la kuleta tija” alisema Loata Sanare.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Loata Ole Sanare akifungua kikao cha kwanza cha Baraza Kuu la Nne la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA).

Mkuu huyo wa Mkoa amesema, bila ushirikiano baina ya Mwajiri na Mtumishi ni vigumu Taasisi kutimiza malengo yake, hivyo Serikali bado inaamini kuwa Mabaraza ni kiungo muhim katika kuleta mafanikio hayo huku akisema mabaraza hayo yapo kwa mujibu wa Sheria. Hata hivyo amewatahadharisha watumishi kuwa ni vyema kabla ya kudai maslahi yao, kupima kwanza kiwango cha utekelezaji wa wajibu wao kwa mwajiri.

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania Prof. Carolyne Nombo (kushoto) akimkaribisha Mgeni  rasmi alipowasili katika viwanja vya Tafori

Loata Sanare amesema kupitia Mabaraza yaliyopo kwenye Taasisi, Waajiri wataweza kupokea maoni ya watumishi na kuweza kufikia maamuzi sahihi ya namna ya kuboresha mazingira ya kazi na watumishi kwa jumla.

Ameongeza kuwa wajibu wa Mabaraza hayo kama vyombo vya ushauri na usimamizi ni kuhakikisha kuwa waajiri na watumishi wanatambua wajibu na haki zao na kuzingatia maadili ya Utumishi ili kuleta tija kwa watumishi, Waajiri na Watanzania kwa jumla.


Baadhi ya Wajumbe wa Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa TIA wakiwa wanaimba wimbo wa "Mshikamano" bila kushikana mikono kwa sababu ya ugonjwa wa COVID 19.

Katika hatua nyingine Loata Sanare kwa niaba ya Waziri Philip  Mpango ameipongeza Taasisi ya TIA kwa mafanikio makubwa waliyofikia katika kutoa Elimu yenye ubora ambayo imechangia kupata wataalamu wanaochangia katika Ujenzi wa Taifa la Tanzania.

Mwisho, amewataka Wakurugenzi, Mameneja wa Kampasi, Wakuu wa Vitengo na Idara kusimamia suala la maadili katika sehemu zao za kazi wakikumbuka kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kuondoa vitendo vyote vya rushwa mahali pa kazi.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania Prof. Carolyne Nombo akimkaribisha Mgeni  rasmi kufungua kikao hicho amesema majukumu makuu ya TIA ni kutoa mafunzo, ushauri wa kitaalam  na kufanya tafiti timizi kwenye Nyanja za Uhasibu, Ununuzi na Ugavi na maeneo mengine ya Biashara.

Prof. Nombo akimkaribisha Mgeni Rasmi kufungua kikao cha wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa TIA

Prof. Nombo amesema, utafiti unaofanywa na TIA kwenye baadhi ya Halmashauri hapa nchini, una mchango katika ukusanyaji wa mapato kwa kuwezesha Halmashauri hizo kuibua vyanzo vipya vya mapato na kubaini namna bora ya kudhibiti upotevu wa mapato kutokana na ukwepaji kodi na ushuru.

Aidha amesema, katika kikao hicho wajumbe wa Baraza hilo watapata fursa ya kupitia maazimio ya kikao cha Baraza lililopita, kuangalia mafanikio  na kuweka vipaumbela kwa mwaka wa fedha 2020/2021 pamoja na kujadili changamoto zinazowakabili na kupata  majibu ya changamoto hizo.


Taasisi ya Uhasibu Tanzania ilianzishwa kwa lengo la kutoa mafunzo, Ushauri na kufanya utafiti kwenye maeneo ya Uhasibu, Ununuzi na Ugavi na maeneo mengine ya kibiashara.

Hadi sasa Taasisi hiyo ina jumla ya wananfunzi 18,717 katika Kampasi zote sita hapa nchini ambazo ziko katika Mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya, Singida, Mwanza, Kigoma na Mtwara.


MWISHO

 


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.