• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Maafisa Ugani Morogoro Waaswa

Posted on: July 3rd, 2020

Maafisa Ughani Morogoro Wapewa ushauri wa bure

Na Andrew Chimesela – Morogoro

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewataka Maafisa Ugani Mkoani humo kushirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine – SUA kutoa Elimu ya kilimo cha kisasa kinacholenga kuzalisha mazao mengi katika eneo dogo ili kuongeza tija kwa wakulima katika  Halmashauri zao.

Mhandisi Kalobelo ametoa ushauri huo Julai 2 mwaka huu wakati wa maadhimisho ya siku ya wakulima ya Mradi wa RIPAT – SUA yaliyofanyika katika Kijiji cha Mlali Wilayani Mvomero ambapo wadau mbalimbali wa sekta ya Kilimo walishiriki.

Mhandisi Kalobelo amesema moja ya sababu ukiachia mbali kupata mazao mengi katika eneo dogo bado teknolojia hiyo inasaidia kupata mazao yaliyobora tofauti na mazao yanayopatikana kwa kutumia kilimo cha kawaida, hivyo amesema ni vema Maafisa Ugani wa kila Halmashauri kuchukua Elimu hiyo inanyotolewa kupitia Mradi wa RIPAT – SUA na kwenda kuisambaza kwa wakulima katika Halmashauri zao.

Hata hivyo Mhandisi Kalobelo amesema wakati umefika sasa kwa kila mmoja hususani wakulima kuanza kukitumia ipasavyo Chuo Kikuu cha SUA ili kupewa mbinu za namna ya kuongeza tija zaidi katika mavuno.

“Nadhani ni wakati sasa kwa  kila mmoja wetu, kuona umuhimu wa kuwatumia wataalamu wetu wa kutoka Chuo Kikuu cha Sokoine kuweza kuona wanatuongezea tija namna gani katika uzalishaji wetu katika mazao mbalimbali” alisema Mhandisi Kalobelo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo akiongea na wanakikundi cha TUKALEGOYA (hawapo pichani) alipotembelea shamba darasa la kikundi hicho

Akiongea na vikundi mbalimbali vya wakulima, Katibu Tawala huyo amewataka wakulima ambao wako kwenye mradi wa RIPAT – SUA kutumia teknolojia ya kilimo waliyoipata kupitia miradi mbalimbali inayofadhiriwa kupitia Chuao Kikuu cha SUA na sehemu nyingine kuwa ni  nyenzo ya madhubuti kwao na jamii inayowazunguka badala ya teknolojia kuitelekeza mara mradi unapokoma.

“Tuna tatizo sisi watanzania wakati mwingine tunafundishwa kweli na tunajifunza kweli lakini tukisha toka hapa inakuwa kama maigizo sasa tusifanye Elimu tuliyoipata hapa iwe ya maigizo, twendeni tukaifanyie kazi. Aliongeza Kalobelo.

 

Mhandisi Kalobelo akipata maelezo ya utendaji kazi wa vikundi kutoka kwa Mtaalamu kutoka Chuo Kikuu cha SUA

Aidha, Katibu Tawala huyo amewatoa wasiwasi wakulima hao kuhusu changamoto ya kupata masoko ya mazao wanayozalisha ikiwemo viazi lishe na kuwataka kuendelea kuzalisha kwa wingi kwani Serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli ni sikivu iko tayari kulinda masoko ya mazao yao hata kwa kutunga sheria ndogo.

Mhandisi Kalobelo akiangalia aina ya maharagwe ambayo kilimo chake kina tija kwa wakulima kwa kuwa yana tabia ya kuzaa sana

Naye Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha SUA Prof. Raphael Chibunda pamoja na kuwataka wanavikundi ambavyo viko kwenye mradi wa RIPAT – SUA kuacha mazoea ya kutelekeza teknolojia wanayopata bado amewaahdi wanakikundi cha TUKALEGOYA cha kijiji cha Mkuyuni Wilayani Mvomero pampu ya kumwagilia baada ya kuonekana ni changamoto kwao.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha SUA Prof. Raphael Chibunda akitoa nasaha zake kwa wanakikundi cha mradi wa RIPAT - SUA. katikati ni Mratibu wa Mradi huo Dk. Emmanuel Malisa

Kwa upande wao Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mvomero Rehema Mhalule akimwakilisha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro waliowawakilisha Wakurugenzi katika hafla hiyo kwa kuwa mradi huo unatekelezwa ndani ya halmashauri hizo wameshukuru mradi huo kuongeza Elimu kwa wakulima wao na kwamba wataendeleo kutoa ushirikiano unaohitajika na kuendeleza mradi huo hata baada ya kufikia kikomo.

Wanakikundi cha Tukalegoya wakiwakaribisha wageni waliowatembelea kwenye shambadarasa lao

Mradi wa Jitihada shirikishi za kuleta mapinduzi ya kilimo  Vijijini  - RIPAT wenye Kaulimbiu “NJAA NA UMASKINI KUWA HISTORIA, INAWEZEKANA” unafadhiriwa na nchi ya Denmark ambao ulianza mwaka 2018 ukikusudia kusaidia jamii kukabiliana na njaa na umaskini.

Hadi sasa Mradi umekwishawafikia wakulima 650 kati ya 720 waliolengwa sawa na 90% kupitia vikundi mbalimbali vya wakulima ambavyo hadi sasa vimefikia 22, wanachama halisi ni 352 ambao wana hisa zenye thamani ya shilingi zaidi ya  milioni 48.

Hili ni moja ya shamba la migomba la wanakikundi cha mradi wa RIPAT - SUA


MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.