• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

KASSIM MAJALI AUNDA TIMU

Posted on: September 16th, 2019

Waziri Mkuu kutuma timu kuchunguza sakata la DC, DED Malinyi

Na. Andrew Chimesela – Mahenge, Morogoro

Kufuatia kuwepo kwa mgogoro wa muda mrefu mkubwa kati ya mkurugenzi wa halmshauri ya wilaya ya Malinyi Musa Mnyeti na mkuu wa wilaya hiyo Majura Kasika waziri mkuu Kassim Majaliwa ameagiza mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za Serikali CAG, Wakala wa Majengo Tanzania TBA na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala bora kufika wilayani humo ili kuchunguza kwa kina kiini cha mgogoro huo.

Waziri Mkuu amesema hayo leo Septemba 16 wakati akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Toboa wilayani Malinyi, ikiwa ni siku ya tatu ya ziara yake ya kikazi mkoani Morogoro.

Waziri Mkuu amefikia hatua hiyo ili kufika katika Wilaya hiyo ili kuchunguza matumizi ya Mapato ya ndani yanayokusanywa katika Halmashauri ya Wolaya ya Malinyi, kukagua majengo yote ya miradi kama yanaendana na thamani ya fedha zilizotumika na kuchunguza chanzo cha maelewano hafifu baina ya Viongozi hao

‘’ Rais anateua viongozi wazuri , waadilifu, wasio wala rushwa, lakini nyie DC na Mkurugenzi wake mmekuja hapa badala ya kufanya kazi mnagombana, nasikia hamuivi chombo kimoja’’ alisema Waziri Mkuu.

Alisema kinachoshangaza viongozi hao wanafikia hatua ya kugombania miradi inayopelekwa na serikali kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na hivyo kusababisha kushindwa kutekelezwa kwa wakati na kwa ukamilifu.

Hivyo, ameamua kumpeleka Wilayani humo CAG, Katibu Mkuu  wa utumishi pamoja na wakala wa udhibiti wa majengo TBA ili kuchunguza na kutoa ripoti pamoja na kuishauri serikali nini kifanyike katika kuchukua hatua.

Amesema ni aibu sana kwa viongozi wa Serikali kuwa na mgogoro baina yenu hadi kufikia hatua ya kuwagawa watumishi, pamoja na wananchi katika kufanya shughuli zao ‘’ Mnakuja hapa hamfanyi kazi, mnagombana hicho mnachokitafuta ole wenu” ameonya.

Awali mbunge wa jimbo hilo Malinyi Dk. Mponda alimwambia Waziri Mkuu kuwa viongozi hao wamekuwa wakirumbana na kugombana waziwazi hali inayosababisha kuzorotesha maendeleo ya wilaya hiyo.

Waziri Mkuu akiwa wilyani Malinyi aliweka jiwe la msingi jengo la Ofisi za Halmashauri ya wilaya hiyo lenye thamani ya shilingi bilioni 3.9 linalojengwa na shirika la nyumba la Taifa NHC na kuwataka vijana wanaopata ajira katika mradi huo kutoharibu miundombinu yake wala kuiba vifaa vya ujenzi wa mradi huo ili waaminiwe .

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • ZAIDI YA BIL. 7 ZATARAJIWA KUTUMIKA MOROGORO.

    March 04, 2021
  • Serikali inapoteza Bil. 18 kwa mwaka

    March 03, 2021
  • Wahasibu Halmashauri za Morogoro waonywa.

    March 03, 2021
  • Mkoa wa Morogoro wajipanga kuwa wa kiutalii.

    February 26, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.