• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Dkt. Kebwe aupiga stop Uongozi wa Kiwanda -Morogoro

Posted on: June 18th, 2019

Dkt. kebwe apiga stop uongozi kiwanda cha magunia – morogoro

Na Andrew Chimesela - Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe ameutaka uongozi wa Kiwanda cha kutengeneza magunia kilichopo Kihonda Mjini Morogoro kusimamisha mara moja zoezi la kutaka kupunguza wafanyakazi wa kiwanda hicho kwa kuwa zoezi hilo halijafahamika vizuri kwa wafanyakazi.

Mkuu wa Mkoa ametoa amri hiyo jana Juni 17 alipofika katika Kiwandani hapo na kufanikiwa kuongea na uongozi wa Kiwanda pamoja na baadhi ya wafanyakazi ambao walikuwa bado hawajaondoka kurudi majumbani kwao huku wakionekana kuwa na wasiwasi na paniki baada ya kusoma matangazo ya kuwepo kwa zoezi hilo la kupunguza wafanyakazi.

Dkt. Kebwe amesema ameamua kuchukua hatua hiyo kwa sababu amepokea simu nyingi pamoja na ujumbe mfupi (sms) kutoka kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho wakilalamikia zoezi hilo kuletwa ghafla na kutojulikana vema maudhui yake.

Dkt. Kebwe amesema kiwanda hicho ndiyo kiwanda pekee katika nchi za Maziwa Makuu hivyo wanakiangalia kwa jicho la pekee na kwa uzito wa hali ya juu kwa sababu hiyo Uongozi wa Mkoa hauwezi kukubali kirahisi mabadiliko ya ghafla na bila uongozi kujua vizuri na hivyo kuamua kusimamisha zoezi hilo.

 “Kwa hiyo waheshimiwa Menejimenti ya kiwanda zoezi hili lisimame kwa sababu halijaeleweka vizuri kwa watumishi na hata sisi ofisini hatulifahamu vizuri”

Akiongea kwa niaba ya wafanyakazi wenzake, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi Kiwandani hapo Bi. Marietha Kazimoto amesema baada ya kusikia taarifa hizo walikwenda kwa uongozi wa kiwanda kuuliza kama Uongozi ngazi ya Mkoa unajua mabadiliko hayo na kujibiwa kuwa hakuna haja ya uongozi huo kujua mabadiliko hayo.

Aidha, Bi. Magreth amesema sababu iliyopelekea wafanyakazi wengi kuwa na wasiwasi ni uharaka wa kufanyika zoezi lenyewe na kwamba baada ya zoezi, wafanyakazi watakaopunguzwa wanaweza kuingia mkataba na kufanyakazi kwa mwekezaji mwingine atakayeendesha kiwanda hicho lakini watatakiwa wawe  na vitambulisho vya NIDA jambo ambalo limewatisha wafanyakazi wengi.

Kwa upande wao wafanyakazi wakiwemo Bw. Richa Stephano, Marcus Mathias na Queen Jackson wamemshukuru Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kuingilia kati zoezi hilo na kwamba wanakubaliana na agizo alilotoa la kusimamisha zoezi hilo hadi pale litakapowekewa utaratibu unaotakiwa ambao hautaeta madhara makubwa kwa pande hizo mbili.

Kutokana na sakata hilo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe ameunda Kamati ya watu Nane (8) ili kuchunguza kwa kina sakata hilo la Uongozi wa Kiwanda kutaka kupunguza wafanyakazi wa kiwanda hicho bila kutoa taarifa za uhakika kwa wafanyakazi wa kiwanda hicho. Kamati hiyo ya watu nane inatarajia kutoa taarifa yake kwa Mkuu wa Mkoa hapo Juni 24, 2019.

Mwisho 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • RC SANARE AIAGIZA TAKUKURU.

    March 13, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.