• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

DKT. KEBWE AUNDA TUME KUCHUNGUZA SHILINGI MIL.76

Posted on: July 3rd, 2018

DKT. KEBWE AUNDA TUME KUCHUNGUZA  SHILINGI MIL.76

Na Andrew Chimesela –Ifakara  Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe ameahidi kuuanda tume ya kuchunguza upotevu wa fedha kiasi cha zaidi ya shilingi 76 Mil. ambazo inasemekana hazijulikani matumizi yake baada ya kutengwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha mabasi cha Kibaoni katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara Wilayani Kilombero.

Dkt. Kebwe ametoa kauli hiyo Julai Mosi mwaka huu muda mfupi kabla ya kuweka jiwe la msingi kwa ajili ya ufunguzi wa  ujenzi wa Kituo kipya cha mabasi cha kibaoni kilichopo katika Halmashauri ya Mji wa Ifakara katika Wilayani Kilombero kilometa tano kutoka kilipo sasa kituo cha mabasi cha zamani cha Mji wa Ifakara.

Amesema, kuna fedha kiasi cha shilingi zaidi ya milioni 76 ambazo miaka ya nyuma inaelezwa zilitumika katika kuendeleza eneo hilo ambalo linatarajiwa kujengwa kituo hicho cha mabasi ingawa matumizi yake hayako wazi, na kwa sababu hizo ni fedha za Serikali haiwezekani kulifumbia macho na kuahidi kuunda tume ili kujua ukweli wake na matumizi yaha hizo.

“Lakini kwa sababu ni hela ya Serikali hatuwezi kufumbia macho…., nitaunda kamati ya kufanya Audit,  wapekuwe waone hele hiyo imetumika vipi na aliyeitumia awe amestaafu au awe amehama ajue hela hiyo ataitapika” alisema Dkt. Kebwe.

Aidha, Dkt. Kebwe ameagiza magari yote ya abiria yanayofanya biashara katika mji wa Ifakara kuanzia Julai 2, mwaka huu yaanze kutumia kituo cha mabasi cha Kibaoni ili kuongeza mapato ya Mji wa Ifakara na amepiga marufuku standi bubu na watakaokaidi agizo hilo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Pamoja na maagizo hayo Kebwe ameutaka uongozi wa Mji wa Ifakara kutowasumbua wafanyabiashara wadogo maarufu kama wamachinga na mama nitilie, badala yake uongozi uwasajili ili watammbulike na kuachwa wafanye biashara zao katika soko hilo wakiwa huru. Aidha,  ameupongeza uongozi huo kwa kutenga vyumba nane kwa ajili ya watu wenye mahitaji Maalum wakiwemo wazee ili kuendesha shughuli zao kwa lengo la kujiongezea kipato kupitia vyumba hivyo. Dkt Kebwe ameuagiza uongozi kutoa yvumba hivyo bure kwa kundi hilo.

Aidha, Dkt. Kebwe amesema ameunda kamati ya kufuatilia sakata la kugawana mali baina ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero na Halmashauri ya Mji wa Ifakara. Taarifa ya Kamati hiyo aliyoiunda imemaliza kazi yake na italetwa na kusomwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro mbele ya viongozi wa Halmashauri zote mbili na hakutakuwa na mjadala katika maamuzi yaliyomo kwenye taarifa hiyo kwa kuwa taarifa imefuata mwongozo uliotolewa na Serikali unavyoelekeza namna nzuri ya kugawana mali hizo.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero James Ihunyo pamoja na kukubaliana na ujenzi wa kituo cha mabasi cha Kibaoni, ameutaka Uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuendelea kuweka fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha mabasi cha kisasa na cha kudumu kwa kuwa kituo cha Kibaoni baada ya kukamilika kwa barabara ya Kidatu - Ifakara hakitafaa tena kwa kuwa kutakuwa na watu na magari mengi kuliko ilivyo sasa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara Mhe. Mashaka Mbilinyi amesema pamoja na kuwa mradi wa Kituo cha mabasi cha Kibaoni utaiingizia mapato Halmashauri yao bado alimemwomba Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kufuatilia mradi huo kwa karibu zaidi hususan matumizi ya shilingi Mil. 76.2 zilivyotumika siku za nyuma, huku Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Francis Ndulane akieleza lengo la mradi huo kuwa ni kupunguza msongamano wa magari katikati ya Mji wa Ifakara na kuzuia standi zisizo rasmi katikati ya Mji huo.

Mradi huo wa Kituo cha Mabasi Kibaoni ni mradi uliopokelewa na Halmashauri ya Mji wa Ifakara kutoka kwa Halmashauri mama ya Wilaya ya Kilombero, na eneo nzima lina ukubwa wa mita za mraba 8,550.

Matangazo

  • Karibu kuwekeza Morogoro April 17, 2018
  • Fomu za Kujiunga Kidato cha Tano kwa Shule za Sekondari za Serikali Tanzania Bara.. June 19, 2018
  • ORODHA YA HATI ZILIZO TAYARI WIZARA YA ARDHI.. August 29, 2018
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA December 14, 2018
  • View All

Habari Mpya

  • Dkt. Kebwe watuliza Wakazi Mindu

    February 21, 2019
  • Waziri Kakunda Atoa Wito Kwa Watanzania

    February 17, 2019
  • Uchimbaji wa Madini

    February 12, 2019
  • Vitambulisho vya Wajasiliamali

    February 04, 2019
  • View All

Video

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa azungumzia mradi wa umeme rufiji
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2018 Mkoa wa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa