• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Mkoa wa Morogoro
Mkoa wa Morogoro

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Maelezo ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu na Vitengo
      • Utawala na Rasilimali
      • Serikali za Mitaa
      • Uhasibu na Fedha
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za maji
      • Miundombinu
      • Huduma za Ugani
      • Elimu
      • Sheria
      • TEHAMA
      • Afya
  • Wilaya
    • Morogoro
    • Mvomero
    • Gairo
    • Kilosa
    • Kilombero
    • Ulanga
    • Malinyi
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Morogoro
    • Morogoro DC
    • Mvomero
    • Gairo
    • Ulanga
    • Malinyi
    • Kilombero
    • Ifakara Mji
    • Kilosa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo Mbalimbali
    • Majarida
    • Fomu Mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha

Bakaa yamchefua RAS Morogoro

Posted on: October 8th, 2020

Bakaa yamchefua RAS Morogoro, ataka hali hiyo kukomeshwa.

Na Andrew Chimesela, Morogoro.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo amewataka Maafisa Mipango na Wachumi Mkoani humo kutoendekeza mazoea ya kutotumia kwa wakati fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na kusababisha fedha hizo kuvuka mwaka au  kurudishwa hazina hivyo kutowatendea haki wananchi.

Mhandisi Kalobelo ametoa onyo hilo Oktoba 8 mwaka huu wakati akifungua Kikao cha Maafisa Mipango, Wachumi na Watakwimu wa Sekretarieti ya Mkoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa Mkoani humo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Veta katika Mji mdogo wa Mikumi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emmanuel Kalobelo (katikati) akisisitiza jambo wakati wa kufungua kikao cha Maafisa Mipango, Wachumi na Watakwimu, kilichofanyika VETA katika Mji mdogo wa Mikumi, Oktoba 8 mwaka huu. Picha na Andrew Chimesela

Amesema, kuna kasi isiyoridhisha kwa baadhi ya Maafisa Mipango na Wachumi ndani ya Mkoa huo katika utumiaji wa fedha za miradi ya Maendeleo hali inayoplekea kuwa na Bakaa kubwa wakati wa mwaka wa fedha unapofika.

“kumekuwa na kasi isiyoridhisha katika matumizi ya fedha za maendeleo hali inayopelekea kuwa na bakaa kubwa wakati wa mwaka wa fedha unapofikia mwisho, kwa mfano, hadi mwisho wa mwaka wa fedha 2019/2020 kulikuwa na Bakaa iliyokuwa inafikia shilingi 9,430,444,666.00 kimkoa” alisema Kalobelo.

Amesema, kutotumia fedha za Serikali kwa wakati kama zilivyoelekezwa na Serikali ni kuwakosea haki wananchi na kupunguza thamani ya fedha zilizotolewa, kwa kuwa fedha hizo zikivuka mwaka hazitatekeleza mradi  kama ilivyopangwa na kushusha thamani ya mradi wenyewe hivyo amewataka Maafisa hao kujipanga kukomesha changamoto hiyo.

Katika hatua nyingine Mhandisi Kalobelo, amewataka Maafisa hao kuwa na nidhamu katika kutekeleza maelekezo wanayopewa na viongozi wao hususan katika suala nzima la uwasilishaji wa taarifa mbalimbali, kwa kuwa baadhi yao wamekuwa na mazoea ya kuwasilisha taarifa hizo nje ya muda waliopewa na kusababisha adha kwa watumishi wengine na Serikali kwa jumla.

Wachumi kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Morogoro wakisikiliza kwa makini Hotuba ya mgeni rasmi ambaye ni Katibu Tawala wa Mkoa huo

Kuhusu uwasilishaji wa maombi ya fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri zao kwa mwaka 2020/2021, Mhandisi Kalobelo ameagiza kila Halmashauri kuwasilisha taarifa hiyo kabla au ifikapo Oktoba 15 mwaka huu, na Afisa ambaye hatawasilisha taarifa hiyo tarehe iliyotajwa atachukuliwa hatua za kinidhamu.

“ikifika tarehe 15 mwezi huu wa kumi 2020, Afisa Mipango yeyote ambaye atakuwa hajawasilisha hiyo taarifa mkoani kwangu nitachukua hatua kali za kinidhamu za uzembe, haiwezekani tuwe tunafanya kazi kwa ratiba zetu sisi wenyewe” alisisitiza Mhandisi Kalobelo.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi, Idara ya Mipango na Uratibu Mkoa wa Morogoro ANZAAMEN NDOSSA amesema, lengo la kikao hicho pamoja na mambo mengine kimelenga kukumbushana majukumu ya Maafisa mipango, Wachumi na Watakwimu, kutathmini utendaji wa kazi na kujifunza mbinu mpya za kuibua miradi yenye tija katika jamii.

Kuhusu changamoto ya bakaa, pamoja na kuiomba Serikali kupeleka  fedha za Maendeleo mapema zaidi, Ndossa amesema Wizara ya Fedha imetoa mwongozo mpya wa namna ya kuomba fedha hizo, hivyo katika kikao hicho wataupitia mwongozo huo na kujipanga kuutekeleza mapema ili kuondoa changamoto ya kubakiza fedha zinazotolewa na Serikali unapofika mwisho wa mwaka wa fedha.

Nao washiriki wa kikao hicho akiwemo Jibril Mandari ambaye ni Mtakwimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero amekiri kupokea agizo la Katibu Tawala wa Mkoa la kutovusha fedha za miradi kutoka mwaka mmoja wa fedha hadi mwaka unaofuata kwa kuimarisha zaidi ushirikiano wa kikazi baina ya Ofisi ya Mhandisi, Afisa Mipango na Ofisi ya Manunuzi kwa sababu Ofisi  hizo ndizo zinazohusika kwa karibu kwenye masuala ya fedha za maendeleo.


Baadhi ya Washiriki wakiwa kwenye kikao hicho

Wakati huo huo Msifwaki Haule ambaye ni Afisa Mipango, ameelza sababu ya fedha kuvuka mwaka kuwa mara nyingi fedha zinazobaki ni zile zinazoletwa na Serikali mwishoni mwa mwaka yaani mwezi Juni pamoja na uwepo wa taratibu za nyingi za kimanunuzi, hata hivyo amekikiri kuyapokea na kuyafanyia kazi maagizo yaliyotolewa na kiongozi wake.

Hii ndio Injini ya Mkoa wa Morogoro ambao wamejificha Mji mdogo wa Kitalii Mikumi, kwa lengo la kuweka mikakati ya namna ya kuupeleka mbele Mkoa wa Morogoro. Kutoka kushoto waliokaa ukimuacha mgeni rasmi, ni Mtakwimu Mkoa wa Morogoro, Anzaamen David Ndossa(Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu), Afisa Mipango wa Halmashauri ya Kilosa Bw. Kaunda, na Jacob Kayange ambaye ni Mchumi kutoka Sekretariet ya Mkoa wa Morogoro

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU(MOCK) KIDATO CHA NNE MEI-2019 MOROGORO July 29, 2019
  • Karibu kuwekeza Mkoani Morogoro September 26, 2019
  • Ifahamu Miongozo ya uazishwaji wa minada ya mifugo, uuzaji wa mifugo katika minada, ukusanyaji wa mapato kupitia minada, nyaraka zinazohitajika katika kusafirisha mifugo n.k Bofya hapa.. February 14, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUGA NA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2020 - MKOA WA MOROGORO December 07, 2019
  • View All

Habari Mpya

  • Morogoro kumuenzi JPM kwa kudumisha Amani na Utulivu.

    March 24, 2021
  • RC MSTAAFU STEVEN MASHISHANGA ATOA SALAMU ZA POLE.

    March 19, 2021
  • RC Sanare awapa pole Wanamorogoro kwa Msiba Mkubwa, awataka watulie

    April 28, 2021
  • RC SANARE AIAGIZA TAKUKURU.

    March 13, 2021
  • View All

Video

Anayetaka kumuheshimu Rais amuheshimu Mwananchi - RC Sanare
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Maelezo ya Mkoa
  • Tangazo la Zabuni
  • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
  • Hotuba
  • Taarifa kwa Umma

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Tanzania
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • TAMISEMI
  • Ikulu
  • Katibu Mkuu Kiongozi
  • Tovuti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki © 2020 Ofisi Ya Mkuu wa Mkoa Morogoro. Haki Zote Zimehifadhiwa.