JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
   
     
     
 
     
TAARIFA YA MKAGUZI
 
[ Nyumbani ]
 
Utangulizi
Kimsingi kazi za Mkaguzi wa Ndani na zile za Mkaguzi wa Nje hazitofautiani kwani wote wawili wanafanya ukaguzi wa mahesabu, ili kuhakikisha ufanisi kiutendaji na matumizi bora ya fedha na mali za Sekretarieti ya Mkoa/Halmashauri. Tofauti iliyopo ni kwamba Mkaguzi wa Ndani ni mtumishi wa Sekretarieti ya Mkoa/Halmashauri na anawajibika kwa Sekretarieti ya Mkoa/Halmashauri kiutendaji, wakati Mkaguzi wa Nje ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na ambaye anawajibika kwa Bunge.

Madhumuni ya Ukaguzi wa Ndani:
  • Kuhakikisha kuwa wakati wote kumbukumbu na nyaraka za uhasibu mahali popote zilipo, zinatayarishwa kwa usahihi na kwa wakati unaostahili
  • Kuhakikisha kuwa uwezekano wa wizi, upotevu na ufujaji wa fedha na mali unadhibitiwa mapema, kwa kufuata taratibu za uhasibu na kanuni za fedha.
  • Kusaidia utendaji mara kwa mara kwa kutathmini taratibu za fedha ili kuhakikisha kuwa zinafaa kwa wakati uliopo na zinakidhi makusudi ya kuwepo taratibu hizo.

 

 
[ Nyumbani ]
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, TEL: 026 - 2604237/2600973, FAX: 026 2601000