JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
     
 
     
  Orodha [ Nyumbani ]
 
MATANGAZO
01.

Kikao cha Bunge Kamati ya Katiba,Sheria na Utawala kujadili na kupitisha mapendekezo ya bajeti ya Mwaka 2009/10 tarehe 4/6/2009 – 5 /6/2009 katika ukumbi wa Karimjee Dar es Salaam .

02.

Kikao cha Baraza la wafanyakazi kitafanyika tarehe 6/06/2009 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Baraza hili limeanzishwa kwa mujibu wa agizo la Rais la mwaka 1970. Lengo la agizo hilo ni kushirikisha Wafanyakazi katika Uongozi wa pamoja mahali pao kazi.

Aidha, ni kwa mujibu wa kifungu cha 30(3) cha Sheria Na.19 ya majadiliano ya mwaka 2003, ikisomwa pamoja na kifungu Na.108 cha kanuni za utumishi wa Umma za mwaka 2003.

Kimsingi, tunapaswa kufanya kikao cha Baraza hili mara mbili (2) kwa mwaka. Pamoja na mambo mengine, wajumbe watapaswa kupitia maeneo ya vipaumbele vya Bajeti ya Mkoa chini ya uenyekiti wa Katibu Tawala Mkoa.

03

Timu ya wataalam (RMT) itakaa tarehe 8/06/2009 kwa madhumuni ya kupitia na kuhakiki ajenda zote zitakazowasilishwa kwenye kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa(RCC) iliyopangwa kufanyika tarehe 11/06/2009.

 

04

Kikao cha kuptia bajeti ya 2009/2010 (Post budget Scrutinizing Review Meeting) na Mwelekeo wa Mkoa kitafanyika tarehe 09/06/2009.

Madhumuni ya kikao hiki ni kuwapatia wajumbe taarifa ya makisio ya bajeti,muelekeo na kuona jinsi gani bajeti ijayo itaweza kutekeleza Sera za Serikali,Malengo ya MKUKUTA,Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 ,Malengo ya Milenia na Dira ya Taifa ya mwaka 2025.

05

Kikao cha Bodi ya Barabara (Road Board) kitafanyika tarehe 10/06/2009.Madhumuni ya kikao hiki ni kupata taarifa za utekelezaji wa kazi zilizo chini ya Wakala wa Barabara nchini(TANROAD) mkoa wa Morogoro.

06

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa(RCC) kitafanyika tarehe 11/06/2009.

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa ni kikao cha kisheria kwa mujibu wa sheria Na.19 ya mwaka 1997 ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Madhumuni ya kikao hiki ni Serikali kukutana na Wadau wote wa maendeleo kujadili maendeleo ya Mkoa

 

07

• Vikao vya Halmashauri Kuu ya CCM (M)

• Kamati ya Siasa ya Halimashauri Kuu ya Mkoa tarehe 25/06/2009

• Halmashauri Kuu(M) Maalum kupokea Utekelezaji wa Ilani ya CCM na Utekelezaji wa Agizo la Rais,Mkoa wa Morogoro kuwa ghala la Chakula la Taifa(FAMOGATA) tarehe 27/06/2009.

Hivi ni vikao vya kiutendaji kwa taratibu za Chama Cha Mapinduzi na kwa ajili kupokea taarifa za utekelezaji kwa mujibu wa maelekezo ya Ilani ya Uchaguzi.

   
   
   
 
Orodha [ Nyumbani ]
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, TEL: 026 - 2604237/2600973, FAX: 026 2601000