Wilaya ya Ulanga ipo kusini mwa Mkoa na ya kwanza kwa ukubwa kimkoa yenye eneo la kilometa za mraba 24,560 ambazo ni sawa na hekta 2, 456,000 pia Wilaya ni ya sita kwa ukubwa kitaifa. Wilaya ipo Kusini mwa Mkoa huu, kwa upande wa Mashariki imepakana na Wilaya ya Liwale katika Mkoa wa Lindi. Upande wa Kusini imepakana na Namtumbo katika Mkoa wa Ruvuma na Kaskazini Wilaya jirani ya Kilombero. Makao Makuu ya Wilaya ni Mahenge ambao upo umbali wa kilomita 312 kusini mwa Mji wa Morogoro.
|