JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
     
 
     
ELIMU
 
[ Nyumbani ]
 

Sekta hii kama ilivyoanishwa kwenye sera ya elimu ya mwaka 1995 msisitizo umewekwa kwenye elimu ya awali, Msingi,Sekondari na elimu ya juu.

Elimu ya Awali

Mkoa umepata mafanikio katika elimu ya awali kwa kuwa na madarasa 626 (2008) ukilinganisha na madarasa 326 yaliyokuwepo mwaka 2005. Pia umeandikisha wanafunzi 30,140 (2008) ikilinganishwa na mwaka 2005 ambao walikuwepo wanafunzi 22,971.

Jedwali la: Elimu ya Awali

 Kiashiria

2005

2008

Ongezeko

asilimia

Idadi ya madarasa

 326

626

92.02

Wanafunzi

22,971

 30,140

31.21

Walimu

 508

 683

34.44

Elimu ya Msingi

Shule za Msingi zimeongezeka toka 757 mwaka 2005 hadi 814 mwaka 2008 sawa na ongezeko la asilimia 7.5.Hali kadhalika madarasa yameongezeka toka 2,092 mwaka 2005 hadi 4,919 mwaka 2008. Aidha, wanafunzi walioko shule za msingi waliongezeka toka 379,079 mwaka 2005 hadi 435,375 mwaka 2008 sawa na ongezeko la asilimia 14.8.

Mafanikio pia yamepatikana baada ya Mkoa kuwa wa 20 kati ya mikoa 21 mwaka 2005 na kufanya vizuri miaka miwili mfululizo ambapo mwaka 2007 umekuwa wa 7 kati ya 21 na mwaka 2008 wa 9 kati ya mikoa 21 Tanzania Bara. Katika ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba.

Mdondoko(dropout) umepungua kwa asilimia 52.2 toka wanafunzi 2,022 mwaka 2005 hadi wanafunzi 966 mwaka 2008.

Jedwali Na.2: Elimu ya Msingi.

Kiashiria

2005

2008

Ongezeko asilimia

Idadi ya Shule

757

814

7.5

Idadi ya madarasa

2,092

4,919

135.1

Idadi ya wanafunzi darasa la I-VII

379,093

435,375

14.8

Uandikishaji Wanafunzi darasa la I

20,966

58,975

181.3

Idadi ya Walimu

7,965

8,913

11.9

Uwiano wa walimu kwa wanafunzi

48

49

2.1

Waliofanya mtihani darasa la saba

20,966

53,413

 

60.7

Waliofaulu

11,669

29,995

157

Mdondoko

2,022

966

52.2

Vyoo

6,198

6,363

2.7

Madawati

97,181

112,592

15.9

Wastani wa ufaulu na nafasi kitaifa

55.7 (20/21)

56.1

(9/21)

0.72

Nyumba za walimu

1,658

1,661

0.2

Chanzo: Taarifa za Wilaya 2005-2008

Elimu ya Msingi kwa walioikosa (MEMKWA ).

Mkoa umefanikiwa kuanzisha vituo vya MEMKWA 781 mwaka 2008 ukilinganisha na

696 mwaka 2005. Pia umeweza kuongeza idadi ya wanafunzi kutoka 4,926 (2005) hadi

7,080 (2008) na kuwa na walimu 1,562 (2008) ukilinganisha na 1,392 mwaka 2005.

Mafanikio haya yanaashiria kuongezeka kwa kiwango cha wanaojua kusoma na

kuandika.

 

Jedwali Na.3: MEMKWA.

Viashiria

2005

2008

Ongezeko asilimia

 

Idadi ya Vituo

696

781

12.21

Wanafunzi

4,926

7,080

43.73

Walimu

1,392

1,562

12.21

Chanzo:Taarifa za Wilaya 2005-2008

2.3. Elimu ya Sekondari

Mwaka 2008 jumla ya wanafunzi 29,995 walifaulu mtihani wa darasa la saba ikilinganishwa na mwaka 2005 ambapo walifaulu wanafunzi 11,669 sawa na ongezeko la asilimia 157.

 

Idadi ya shule za Sekondari zimeongezeka kutoka shule 58 (2005) hadi 180 (2008). Aidha madarasa yameongezeka kutoka madarasa 418 (2005) hadi 763 (2008), wanafunzi wa sekondari waliongezeka kutoka 23,643 (2005) hadi 39,495 (2008).

Mafanikio mengine ni kama yaliyoonyeshwa katika jedwali Na. 4 – elimu ya sekondari.

Jedwali Na.4: Elimu ya Sekondari

Kiashiria

2005

2008

Ongezeko

asilimia

Idadi ya Shule

58

180

210.3

Idadi ya madarasa

418

763

82.5

Idadi ya wanafunzi kidato cha I-IV

23,643

39,495

67.0

Idadi ya Walimu

1,098

1,848

68.3

Waliofanya mtihani darasa la saba

20,966

53,469

155.0

Waliofaulu

11,669

29,995

157.0

Chanzo: Elimu taarifa za Wilaya 2005 -2008

 

         
 
[ Nyumbani ]
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, TEL: 026 - 2604237/2600973, FAX: 026 2601000