JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
     
 
     
BARABARA NA MAJENGO
 
[ Nyumbani ]
 

Mtandao wa barabara za Mkoa

Mkoa wa Morogoro una mtandao wa barabara zenye jumla ya urefu wa km.3, 000,kati ya hizo km.1,627.92 ziko chini ya TANROAD na km.1,372.08 ziko chini ya Halmashauri za Wilaya na Manispaa.

Jedwali la Barabara za Mkoa wa Morogoro.

S/N

 

Aina ya Barabara

Urefu

Aina ya Barabara Urefu(Km)

Km nzuri

Km nzuri kiasi

Jumla

   

KM

Lami

Changarawe

 

1

Barabara Kuu

557.00

557.00

557.00

557.00

557.00

2,785.00

2

Barabara za Mkoa

1,069.40

1,069.40

1,069.40

1,069.40

1,069.40

5,347.00

3

Barabara za Wilaya

2,593.00

2,593.00

2,593.00

2,593.00

2,593.00

12,965.00

4

Barabara za Mjini

269.80

269.80

269.80

269.80

269.80

1,349.00

5

Barabara za Jamii

1,099.00

1,099.00

1,099.00

1,099.00

1,099.00

5,495.00

6

Njia za Miguu

219.00

219.00

219.00

219.00

219.00

1,095.00

 

Jumla

5,807.20

5,807.20

5,807.20

5,807.20

5,807.20

29,036.00

Chanzo: Wakala wa Barabara Mkoa ,2008.

11.2 Mafanikio ya matengenezo ya barabara Mkoani ni kama ifuatavyo:

Barabara ya Mziha – Magole – Kilosa hadi Mikumi

Serikali imepania kujenga barabara ya lami kati ya Mziha – Magole – Kilosa – Mikumi na hadi sasa upembuzi yakinifu umekamilika na barabara hiyo kuimarishwa ili iwekwe lami. Serikali inaendelea na juhudi za kuhakikisha barabara hiyo inawekwa lami.

Barabara ya Ifakara – Taweta

Sehemu ya barabara ya Mpanga - Taweta yenye urefu wa km 34 ilifunguliwa mwaka 2006/2007; baada ya matengenezo makubwa

Barabara ya Mvomero – Ndole (Maskati Jct) – Kibati – Lusanga

Barabara hii imekwisha tengenezwa katika sehemu korofi za Matale hadi Ndole na kupitika kwa mwaka mzima.

 Usanifu wa Daraja la Mwere/DDC

Usanifu wa Daraja la Mwere/DDC umefanywa na TanRoads ili kupunguza msongamano wa magari yanayotoka katikati ya mji kuelekea posta. Mkoa unatafuta fedha za ujenzi wa daraja hili.

Daraja la Mto Kilombero

Upembuzi yakinifu na usanifu wa awali wa daraja la mto Kilombero umekamilika ili kujenga daraja hilo. Hatua za maandalizi ili ujenzi uanze zinaendelea.

Daraja la Mto Sagamaganga

Daraja limejengwa na kukamilika hivyo kuwaondolea kero wananchi wa Wilaya ya Kilombero na Uranga.

Daraja la Mto Mwatisi

Usanifu wa daraja hili umekamilika na hatua za kukamilisha ujenzi zinaendelea.

Barabara ya Ifakara Mjini

Ujenzi wa Km 7 za barabara ya Ifakara mjini kwa kiwango cha Lami umekamilika na hivyo kuboresha usafiri na maisha ya wananchi.

12.0. UJENZI WA MAJENGO YA SERIKALI

Ukarabati umefanyika kwa nyumba za Wakuu wa Wilaya Ulanga, Kilosa na Kilombero; na nyumba ya Katibu Tawala Wilaya Ulanga.Ujenzi wa jengo na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mvomero upo katika hatua za mwisho ( finishing ). Nyumba ya Mkuu wa Wilaya Mvomero inaendelea kujengwa Pia jengo la ofisi na nyumba ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Mvomero. Watumishi wa Ulanga wamejengewa nyumba mpya na ukumbi wa Mikutano na ujenzi unaendelea.Ukarabati wa jengo Kongwe Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Awamu ya Kwanza imekamilika na jitihada zinaendelea za kukamilisha ujenzi huo.

 

 

         
 
[ Nyumbani ]
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, TEL: 026 - 2604237/2600973, FAX: 026 2601000