JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
 
     
     
 
     
ARDHI, RAMANI NA UPIMAJI
 
[ Nyumbani ]
 

UMBILE LA ARDHI

Umbile la ardhi ya Mkoa wa Morogoro linajumuisha milima ya Uluguru, Ukaguru, Nguru, Udzungwa na Mahenge. Mabonde na tambarare yamegawanywa na mito inayoanzia milimani. Baadhi ya mito hiyo ni Kilombero, Ruaha, Luwegu, Ruvu, Wami, Ngerengere, Mkindo na Mkondoa. Mito hiyo inafaa kutumika kwa kilimo cha umwagiliaji. Kwa ujumla, ardhi ya Mkoa wa Morogoro ni nzuri na inafaa kwa kilimo cha mazao karibu yote yanayolimwa hapa nchini.

VIWANJA

Mwaka 2008 vilipimwa viwanja 8,960, ukilinganisha na viwanja 175 vilivyopimwa mwaka 2005. Pia vijiji vilivyopimwa mipaka vimefikia 458 (2008) ukilinganisha na 263 (2005). Vijiji vilivyobaki kupimwa mipaka ni 85 kati ya 543

Takwimu za utekelezaji sekta ya Ardhi

Shughuli

Ongezeko (%)

 

2005

2008

Upimaji wa Viwanja

1,757

8,960

40 9.96

Upimaji wa Mashamba

23

105

356.52

Kutoa hatimiliki za ardhi za viwanja

358

412

15.08

Kutoa hatimiliki za ardhi za mashamba

 

74

 

Mipango ya matumizi bora ya ardhi

71

101

42.25

Vijiji vilivyopimwa mipaka

263

458

74.14

Chanzo:Taarifa za Wilaya 2005-2008

 

 

         
 
[ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, TEL: 026 - 2604237/2600973, FAX: 026 2601000