Mkoa wa Morogoro ni Mkoa wa kwanza kwa ukubwa hapa nchini. Mkoa una eneo la Kilometa za mraba 73,039. Eneo hili ni sawa na asilimia 7.7 ya eneo lote la Tanzania Bara ambalo ni kilomita za mraba 947,300. Kati ya eneo hili Km 2,240 ni maji. Mkoa umepakana na Mikoa ya Manyara na Tanga upande wa Kaskazini , kwa upande wa Mashariki unapakana na mikoa ya Pwani na Lindi, na kwa upande wa Magharibi umepakana na Mikoa ya Dodoma na Iringa. Upande wa Kusini unapakana na Mkoa wa Ruvuma.
Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisaini Kitabu cha Mahudhurio Ikulu ndogo Morogoro na
pembeni yake ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Joel Bendera. Rais Kikwete alifanya ziara Mkoani Morogoro na kutembelea Chuo Kikuu cha Waislamu ambapo alifanya uzinduzi wa Jengo la ICT. Pia katika ziara hiyo Mh Rais aliongoza Harambee kwa ajili ya Ujenzi wa Kanisa la Parokia ya Kigurunyembe Morogoro, Harambee hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Magadu. Maelezo zaidi bonyeza hapa!!
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh Joel Bendera akimkabidhi zawadi Balozi wa Ireland Nchini (Wa katikati), kushoto kabisa ni Waziri wa Biashara na Maendeleo Nchini Ireland Mh Joe Kastello.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro wakiwa na nyuso za furaha katika kusherehekea siku ya Wanawake Duniani, Sherehe hizo katika Mkoa wa Morogoro ziliadhimishwa Tarafa ya Matombo katika Wilaya ya Morogoro. Matukio Bonyeza Hapa!!