Karibu katika Tovuti ya mkoa wa Morogoro!
Mkoa wa Morogoro ni Mkoa wa pili kwa ukubwa hapa nchini ukitanguliwa na Mkoa wa Tabora. Mkoa una eneo la kilometa za mraba
73,039. Eneo hili ni sawa na asilimia
8.2 ya eneo lote la Tanzania bara.
Mkoa umepakana na Mikoa ya Pwani na Lindi upande wa Mashariki, Manyara na Tanga upande wa Kaskazini, Mikoa ya Dodoma na Iringa upande wa Magharibi na Mkoa wa Ruvuma upande wa Kusini.
Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisalimiana na baadhi ya viongozi na watumishi wa Mkoa wa Morogoro mara baada ya kuwasili jana kwa ziara Mkoani.
Anayepeana naye mkono ni Eden Munisi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, katikati ni Grayson Kikwesha Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu, kulia kabisa ni Benvenut Lopa Katibu Tawala Wilaya ya Mvomero.Rais Kikwete amefanya ziara Mkoani Morogoro Tarehe 29-30/7/2010 na kuhamasisha zoezi la uchangiaji ujenzi wa sekondari ya Ebenezer ya KKKT Dayosisi Morogoro. Maelezo zaidi hapa!!
Luteni Kanali Mstaafu Issa Saleh Machibya Mkuu wa Mkoa Morogoro, akifungua kikao cha Mrejesho wa Bajeti ya 2010/11 katika Ukumbi wa Hoteli ya Morogoro Bonyeza hapa kwa maelezo
Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imewajengea nyumba za kuishi wahanga wa mafuriko Wilaya humo. Nyumba hizo zimejengwa katika maeneo zilizokuwa Kambi hizo. Hayo ni matokeo ya haraka yaliyochukuliwa na Halmashauri hiyo.