Karibu katika Tovuti ya mkoa wa Morogoro!
Mkoa wa Morogoro ni Mkoa wa pili kwa ukubwa hapa nchini ukitanguliwa na Mkoa wa Tabora. Mkoa una eneo la kilometa za mraba
73,039. Eneo hili ni sawa na asilimia
8.2 ya eneo lote la Tanzania bara.
Mkoa umepakana na Mikoa ya Pwani na Lindi upande wa Mashariki, Manyara na Tanga upande wa Kaskazini, Mikoa ya Dodoma na Iringa upande wa Magharibi na Mkoa wa Ruvuma upande wa Kusini.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Morogoro na Wadau mbalimbali wa Sekretarieti ya Mkoa, wakiwa katika picha ya pamoja nje ya Ukumbi wa Edema ambapo wafanyakazi na wadau hao walishiriki mafunzo maalum ya uandaaji wa Mpango Mkakati,
Mafunzo ya Opras kwa watumishi na Mafunzo ya Mkataba wa Huduma kwa Mteja. Mafunzo hayo kwa mara ya kwanza yalishirikisha Watumishi wa ngazi zote katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Pia baada ya mafunzo hayo timu ya wawakilishi itaundwa ili kuhakikisha Mkoa unapata Mpango Mkakati na Huduma kwa Mteja kwa wakati muafaka na watumishi wanajaza fomu za OPRAS kwa ufasaha.
Picha juu Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Bw. Hussein Kattanga akifungua mafunzo kwa Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Morogoro juu ya uandaaji wa Mpango Mkakati, Mkataba wa Huduma kwa Mteja na OPRAS.Bonyeza hapa kwa maelezo
Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa imewajengea nyumba za kuishi wahanga wa mafuriko Wilaya humo. Nyumba hizo zimejengwa katika maeneo zilizokuwa Kambi hizo. Hayo ni matokeo ya haraka yaliyochukuliwa na Halmashauri hiyo.